المشاركات

𝗠𝗢 𝗔𝗠𝗧𝗘𝗨𝗔 𝗠𝗔𝗚𝗢𝗥𝗜 𝗞𝗨𝗢𝗡𝗚𝗢𝗭𝗔 𝗕𝗢𝗗𝗜,𝗕𝗔𝗕𝗥𝗔 𝗔𝗥𝗨𝗗𝗜 𝗞𝗨𝗡𝗗𝗜𝗡𝗜 ,𝗧𝗥𝗬 𝗔𝗚𝗔𝗜𝗡 𝗔𝗣𝗘𝗪𝗔 𝗠𝗞𝗢𝗡𝗢 𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔𝗛𝗘𝗥𝗜

 


Simba imefanya mabadiliko makubwa ya Bodi ya Wakurugenzi baada ya mwekezaji Mohammed Dewji ‘MO’ akijiweka kando, huku akimteua Crescentius Magori kuchukua nafasi hiyo, ilihali CEO wa zamani wa klabu hiyo, Barbara Gonzalez akirejea klabuni.

Mabadiliko hayo ambayo yametangazwa dakika chache zilizopita, MO mbali na Magori aliyewahi kuwa, Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo na mshauri wa Mo Dewji ameteua sura mpya nne, huku watatu wakitoka Bodi iliyopita.



Wajumbe wapya wanne katika Bodi hiyo ni pamoja na mfadhili wa zamani wa Simba, Azim Dewji aliyekuwa Mwenyekiti wa zamani, Swedy Mkwabi, aliyekuwa Ofisa Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez na George Ruhango.

Barbara alitangaza kujiuzulu Simba Desemba, 2022 japo nafasi hiyo ya Mtendaji Mkuu aliiacha rasmi Januari 10, 2023 akiwa mmoja ya viongozi walioweka heshima klabuni hapo, hasa kwa mafanikio ya Simba kimataifa.



Wengine ni Zuly Chandoo, wakati Rashid Shangazi na Hussein Kitta wakiendelea kwenye Bodi hiyo.

Kwenye Uteuzi huo jina kubwa lililoshtua likikosekana ni Salim Mhene ‘Try Again’ aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo.

Taarifa hiyo haijaweka wazi sababu za kuondolewa kwa Try Again ambaye alikuwa Mjumbe aliyedumu kwa muda mrefu kabla ya mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji.

إرسال تعليق

NextGen Digital Welcome to WhatsApp chat
Howdy! How can we help you today?
Type here...