المشاركات

...🚨🚨𝗬𝗔𝗡𝗚𝗔,𝗧𝗙𝗙 𝗪𝗔𝗙𝗜𝗞𝗜𝗔 𝗣𝗔𝗕𝗔𝗬𝗔

BARUA YA YANGA WAMEIYACHA LEO TFF Kwenye barua ya Yanga waliyoipeleka TFF leo ambayo Ujumbe wa Yanga uliongozwa na Mtendaji Mkuu, Andre Mtine na Mkurugenzi wa Fedha wameambatanisha INVOICE takribani tano.

1- Invoice za Ubingwa Federation Cup zipo tatu kuanzia msimu wa 2021/22.

2- Invoice ya Fedha za Mapato ya Mlangoni za Michuano ya CAF ambazo Yanga walikatwa na CAF ambazo TFF hawajawalipa Yanga.

3- Invoice za Udhamini wa timu ya Wanawake na Mashindano ya Vijana.

Yanga pia wamesititiza TFF wapige hesabu zao na wana machaguo mawili baada ya hapo kuhusu Fedha zao

1- Kuweka fedha zote ambazo Yanga wanawadai inakadiriwa MILLION 426 za Kitanzania, kisha TFF watume INVOICE za Madeni yao yote Jangwani kisha Yanga walipe madeni hayo.

2- Kama TFF waliwakata fedha zote ambazo wanadaiwa, Yanga wanataka kujulishwa kwa USHAHIDI WA RISITI kama ambavyo Sheria za Kodi za nchi zinavyotaka kisha baki yao waingiziwe kwenye account yao ila Makato yote yawe na RISITI.
KISHA Yanga Msimamo wao ni kuwa hakuna maongezi yoyote na kama kuna maongezi (Reconciliation) basi Yanga wapo tayari maongezi hayo yafanyike mbele ya TRA na Mamlaka za Usalama kuhusu MADENI ili kumbukumbu zikae sawa. Thats it for now.

إرسال تعليق

NextGen Digital Welcome to WhatsApp chat
Howdy! How can we help you today?
Type here...